MAENDELEO YA VIWANDA

MAENDELEO YA VIWANDA

Sekta ya Viwanda inasimamiwa na Idara ya Maendeleo ya Viwanda chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara. Idara hii ina jukumu kuu la  kusimamia, kuendeleza, na kuweka mazingira bora ya ukuaji endelevu wa sekta ya viwanda nchini.    

Majukumu

Kutoa na kuratibu misaada ya kiufundi katika uundaji, mapitio na kuwezesha utekelezaji wa sera, mikakati, mipango, program na sheria za kuhamasisha maendeleo ya viwanda

Kuwezesha uundaji na uimarishaji wa vyama vya kisekta na kitaifa vya wazalishaji viwandani

Kuhamasisha na kuratibu shughuli za utafiti na maendeleo ya viwandani na kushirikiana na taasisi za mafunzo, sayansi na teknolojia ili kukuza rasilimali watu za stadi zinazofaa.

Kuwezesha utekelezaji wa programu maalum chini ya vitengo vya KAIZEN, TDU, na IIU ili kuboresha maendeleo ya viwanda

Kufuatilia na kutathmini utendaji wa viwanda na utekelezaji wa miradi ya viwanda

Kuwezesha mchakato wa kitaifa wa mashauriano ili kukuza maendeleo ya viwanda nchini

Kutoa misaada ya kiufundi ili kuwezesha uwekezaji katika sekta ya viwanda

Kuandaa taarifa za kina za sekta ya viwanda

Sera & Mikakati

Miradi / Programme

Taasisi zilizo chini ya Wizara

Wasiliana Nasi

  • Wizara ya Viwanda na Biashara
  • Mji wa Serikali, Mtumba, Mtaa wa Viwanda S.L.P 2996, 40478, Dodoma Jengo la Mambo ya Nje 4th Floor Shaaban Robert Street, Dar es Salaam, Tanzania
  • 0
  • 0
  • info@mit.go.tz