Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Habari

NDC KUHAKIKISHA MIRADI YA KIMKAKATI NA KIELELEZO INATEKELEZWA KIKAMILIFU


NDC hakikisheni Miradi yote ya Kimkakati na Kielelezo inatekelezwa kikamilifu 

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo

ameliagiza Shirika la Taifa la Maendeleo(NDC) kuhakikisha miradi yote ya kimkakati na kielelezo ikiwemo Mradi wa Chuma wa Maganga Matitu unaotarajiwa kuanza hivi karibuni  utekelezaji wake unasimamia kikamilifu kwa manufaa ya Taifa.

Ameyasema hayo Julai 29, 2024,  jijini Dar es Salaam alipotembelea NDC kwa lengo la kujenga uelewa wa pamoja kuhusu shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Shirika hilo hususani usimamizi wa utekelezaji wa miradi ya kimkakati na kielezo ya Taifa.

Aidha, amelipongeza Shirika hilo kwa kazi nzuri inalolifanya katika kusimamia miradi ya kimkakati na kielelezo ya Taifa ambayo inalenga  kuviwezesha viwanda kupata malighafi muhimu kama vile chuma magadi soda  na nk kwa urahisi nchini na kupunguza uagizaji malighafi hizo nje ya nchi ili

kukuza  viwanda na uchumi kwa ujumla

"NDC  ni Shirika  kubwa linategemewa na Taifa, ndio roho ya uchumi, tujue tuna dhamana kubwa, hivyo tutapambana pamoja kuhakikisha NDC inafanya vizuri tumsaidie Rais," alisema Dkt. Jafo.

Aidha, ametoa wito kwa Watumishi wa Shirika hilo kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi, ubunifu na ushirikiano  baina yao pamoja na  ili kuendeleza Shirika hilo muhimu na kutimiza malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kujenga uchumi shindani wa viwanda.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa NDC Dkt Nicholaus Shombe akitoa taarifa ya utekelezaji  wa miradi hiyo amesema  Shirika hilo linasimamia miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo Liganga na Mchuchuma, Mradi wa chuma wa Maganga matitu na Magadi soda wa Engaruka

Aidha akielezea Mradi wa Chuma wa Maganga Matitu ambao Mkataba wake na Mwekezaji unasainiwa hivi karibuni ambapo mwekezaji atakuwa na asilimia 64 na Serikali 36

unatarajiwa kuanza kuchimba kiasi cha tani milioni moja kwa mwaka na uzalishaji utaongezeka