Majukumu ya Wizara
Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara imeundwa kwa mujibu wa Hati idhini GN Namba 384 ya mwaka 2022 na Mgawanyo wa majukumu ya ofisi GN Namba 534 ya mwaka 2021 na kupewa majukumu mahsusi ya kisekta kama ifuatavyo: -
-
Kuandaa, kuratibu na kupitia sera na mikakati ya sekta za Uwekezaji, Uwezeshaji wananchi kiuchumi, Maendeleo ya Sekta Binafsi, Ushiriki wa wananchi katika fursa za uwekezaji na miradi ya kimkakati, viwanda, Biashara na Maendeleo ya wajasiriamali;Kuhamasisha uwekezaji wa ndani na nje ya nchi;
-
Kuboresha mazingira ya biashara nchini;
-
Kukuza uwezeshaji kiuchumi na maendeleo ya Sekta Binafsi;
-
Kusimamia ushiriki wa wananchi katika miradi ya kimkakati na uwekezaji;
-
Kusimamia masuala ya Uwekezaji Tanzania;
-
Kusimamia masuala ya Mauzo ya Nje ;
-
Kusimamia maendeleo ya Viwanda na Biashara;
-
Kusimamia maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo (SMEs);
-
Kuratibu na kuendeleza mitaa, maeneo na kongano za viwanda;
-
Kuendeleza miundombinu ya viwanda;
-
Kusimamia miliki bunifu;
-
Kusimamia masuala ya ushindani wa haki;
-
Kusimamia vipimo, viwango na ubora;
-
Kusimamia intelijensia ya masoko na uhamasishaji wa biashara;
-
Kuhamasisha mauzo ya bidhaa nje ya nchi;
-
Kusimamia usajili wa biashara;
-
Kufanya kazi na Taasisi za kimataifa zinazohusiana na Uwekezaji, Viwanda na Biashara;
-
Kuimarisha na kuendeleza ufanisi wa rasilimali watu katika Wizara; na
-
Kusimamia Idara, Taasisi, programu na miradi chini ya Wizara.