Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Majukumu ya Wizara

Wizara ya Viwanda na Biashara imeundwa kwa mujibu wa Hati idhini GN Namba 619A ya mwaka 2023 na Mgawanyo wa majukumu ya ofisi na kupewa majukumu mahsusi  kama ifuatavyo: -

  1. Kuandaa na kufuatilia utekelezaji wa sera na mikakati ya sekta za Viwanda, Biashara na Viwanda na Biashara ndogo;
  2. Kusimamia maendeleo ya Viwanda na Biashara;
  3. Kusimamia maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo (SMEs);
  4. Kuendeleza miundombinu ya viwanda;
  5. Kusimamia miliki bunifu;
  6. Kusimamia masuala ya ushindani wa haki;
  7. Kusimamia vipimo, viwango na ubora;
  8. Kusimamia intelijensia ya masoko na kukuza biashara;
  9. Kukuza mauzo ya bidhaa nje ya nchi;
  10. Kusimamia usajili wa biashara;
  11. Kufanya kazi na Taasisi za kimataifa zinazohusiana na Viwanda na Biashara;
  12. Kuimarisha na kuendeleza ufanisi wa rasilimali watu katika Wizara; na
  13. Kusimamia Idara, Taasisi, Programu na Miradi chini ya Wizara.