Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)

Lengo Kuu

Kitengo cha TEHAMA kina jukumu kubwa la kuiwezesha wizara kufanya kazi zake kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano

Majukumu

  • Kupitia Sera za TEHEMA kwa ajili ya maboresho yake
  • Kusimika miundombinu ya TEHAMA pamoja na kusimamia matengenezo yake.
  • Kutoa mafunzo juu ya matumizi ya mifumo ya TEHAMA.
  • Kushauri matumizi sahihi ya vifaa vya TEHAMA na kusimamia manunuzi ya vifaa hivyo(hardware&software)
  • Kutoa msaada wa kitaalam kwenye matumizi ya vifaa na mifumo ya TEHAMA.
  • Kushauri juu ya usimikaji wa mifumo mipya ya TEHAMA.
  • Kukusanya takwimu na taarifa za viwanda, biashara na masoko ili na kuziweka kwenye mfumo (kanzidata)