Habari
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Ashatu Kijaji akutana na kufanya mazungumzo na Bi Rossella Lyu na ambaye ni Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Kampuni ya GreeChain

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Ashatu Kijaji akutana na kufanya mazungumzo na Bi Rossella Lyu na ambaye ni Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Kampuni ya GreeChain kutoka nchini China inayojihusisha na Biashara ya matunda pamoja na uongezaji thamani bidhaa za kilimo.
Aidha katika mazungumzo hayo yaliyofanyika jijini Dodoma leo tarehe 25/07/2023 Kampuni hiyo imeonesha nia ya kununua na kuuza bidhaa za parachichi kutoka Tanzania kwenda China pamoja na kukusudia kuwekeza Tanzania katika Ujenzi wa Kituo Kikubwa cha kuhifadhia bidhaa za Matunda (COLD ROOMS) Kurasini jijini Dar es Salaam