Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Habari

Tanzania imepiga hatua kuzalisha na kusambaza umeme vijijini


Waziri wa Viwanda na Biashara,Mhe Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amesisitiza  kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuzalisha na kusambaza umeme vijijini na mjini.

Waziri kijaji ameyasema hayo Aprili 29, 2024 alipokuwa akishiriki  Mjadala kuhusu mageuzi ya nishati duniani wakati waMkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani unaloendelea Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Vilevile ametoa wito kwa nchi zilizoendelea kiviwanda kuunga mkono juhudi hizo ili kuimarisha uzalishaji viwandani.

Dkt kijaji anaongoza ujumbe  wa Tanzania katika mkutano huo unaowajuisha Mkurugenzi wa  Idara ya Maendeleo ya  Biashara Bw. Sempeho Manongi, Mkurugenzi wa Bodi ya Maghala Bw. Asangye Bangu, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa  TanTrade Bw. Deo Shayo, Kamishna wa Fedha za Nje Bw. Rashed Bade na Maafisa Waandamizi wa Ubalozi wa Tanzania- Riyadh Saudi Arabia.