Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Habari

Wahitimu wa CBE waaswa kujiepusha na makundi hatarishi ya Madawa ya kulevya



Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Hashill Abdallah ametoa wito kwa wahitimu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kujiepusha na tabia hatarishi , makundi yasiyofaa ikiwemo matumizi ya  madawa ya kulevya.

Dkt. Hashill ametoa wito huo  kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara (Mb) Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa mahafali ya 58  Kampasi ya Mbeya  katika Ukumbi wa Chuo cha Elimu ya Biashara CBE Iganzo-Mbeya tarehe 2 Desemba 2023.

"Wahitimu zingatieni yale yote mliyofundishwa na kuyafanyia kazi ili yalete manufaa,mnapaswa kuwa wabunifu katika kutumia maarifa mliyopata ili kukabiliana na changamoto mbalimbali na kujiepusha na makundi yasiyofaa na matumizi ya Madawa ya kulevya" Amesema Dkt.Abdallah.

Naye Mwenyekiti wa bodi ya uongozi wa CBE Prof. Wineaster Anderson ameeleza kuwa Kampasi ya CBE Mbeya  imetimiza miaka 10 toka ilipoanzishwa mwaka 2013 na imefanikiwa kununua eneo  jipya lililopo  Iganzo lenye ukubwa wa hekari 54.9 na kujenga miundombinu ya majengo mapya ambayo yanayotumika kufundishia  na kutoa  huduma zingine katika Kampasi ya  Mbeya.

Kwa upande wake Mkuu wa  Chuo cha CBE Prof. Edda Tandi Lwoga katika hotuba  ameeleza  kuwa Chuo kinaadhumisha  maafali ya 58 toka kianzishwa kwake 1965, yakiwa maafali 10 kwa Kampasi ya Mbeya ambapo  ujumla  ya wanafunzi 1008 kati ya 17205 wakitoka  Kampasi ya Mbeya.

Aidha ameeleza kuwa  katika Kampaso ya Mbeya  CBE inatoa kozi  mbalimbali kwa  ngazi za Astashada, Stashahada na Shahada  katika masomo ya  Uhasibu, Uongozi wa Biashara, Masoko, Ununuzi na Metologia ya Viwango