Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Habari

SERIKALI YAZIAGIZA WRRB NA COPRA KUWAWEZESHA WAKULIMA NA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO KUPITIA STAKABADHI ZA GHALA


Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) zimeagizwa kuwa na mkakati wa kuwawezesha wakulima kuanzia uzalishaji ukusanyaji hadi uuzaji ili kuleta tija na bei nzuri ya Mazao.

Vilevile Serikali imetoa rai kwa wakulima na wafanyabiashara kuwa waaminifu na kuunga mkono Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kwa kuimarisha upatikanaji wa pembejeo, mbegu, teknolojia, na masoko ya uhakika ili kuongeza thamani ya mazao ya kilimo, kulinda maslahi ya wakulima, kuongeza ajira na kuimarisha uchumi wa nchi.

Hayo yameelezwa Februari 25, 2026 na Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga,wakati wa hafla ya kufunga msimu wa matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kwa msimu wa 2025/2026 na kufungua msimu mpya wa 2026/2027 iliofanyika mkoani Simiyu.

Aidha ameiagiza, WRRB kutoa elimu na kuwahamasisha wakulima, wafanyabiashara, wasimamizi wa ghala, na wadau wengine muhimu kutumia Mfumo huo pamoja na kiwawezesha wale wenye maghala ambayo hayajakidhi vigezo ili wafanikiwe kutoa huduma bora.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha amesema kufunga na kufungua Msimu wa Mauzo ya Mazao katika Mkoa huo kumekuwa ni chachu na hamasa kwa Wananchi kuendelea kutumia Mfumo huo.

Mkurugenzi wa WRRB, Asangye Bangu, amesema msimu wa 2025/2026 umerekodi mauzo ya tani milioni 1.1 za mazao, ikiwa ni ongezeko la 43% kutoka msimu uliopita. Wakulima wamejipatia Shilingi trilioni 2.4, huku korosho, mbaazi, na ufuta yakiongoza mauzo hayo.

Aidha, Mfumo umepanuka kutoka wilaya 65 hadi 114, waweka mali kutoka 224 hadi 788, mapato ya Halmashauri kufikia Shilingi bilioni 65, ajira zaidi ya 11,430 na leseni za maghala kufulia 286.

Katika msimu wa 2026/2027, WRRB imelenga kuingiza sekta za mifugo, ngozi, na mwani kwenye mfumo wa stakabadhi za ghala na inahimiza Sekta binafsi kuanzisha Maghala bora yanayohamishika.

Nao Watumiaji wa Mfumo huo katika Mkoa wa Simiyu Bw. Daud Mpina na Mariam Litwina wananufaika na Mfumo huo kwa kuuza Mazao yaonkatika Manda kwa uwazi kwa bei nzuri na kupata fedha kwa wakati na Warioba Serikali kuendelea kuboresha Mfumo huo