Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Habari

Waziri wa Viwanda na Biashara  Mhe Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) amesema Serikali itahakikisha inakisaidia Kiwanda cha kutengeneza Vipuri Kilimanjaro ( KMTC)


Waziri wa Viwanda na Biashara  Mhe Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) amesema Serikali itahakikisha inakisaidia Kiwanda cha kutengeneza Vipuri Kilimanjaro ( KMTC) kufikia malengo katika masoko kwa kuwa  dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ni kuona uzalishaji wa ndani unafanyika kupitia chuma kinachozalishwa nchini. 

Amesema hayo Agosti 2, 2023 alipotembelea Kiwanda hicho  kilichopo Mkoani Kilimanjaro kujionea shuhhulizilipo pamoja na kisikiliza na kitatua changamoto zao.

Aidha amewapongeza wafanyakazi wa kiwanda hicho  n kiwataka kuwa   waaminifu kwa kiwa  Serikali inafanya jitihada mbalimbali za kuweka  mazingira bora ya biashara  ili kuvutia wawekezaji katika viwanda vitakavyotumia vipuri vinavyotengenezwa na kiwanda hicho.