Habari
Ziara ya Kamati ya Bunge Viwanda, Biashara na Mazingira Viwandani.

KAMATI YA BUNGE VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA YATEMBELEA KIWANDA CHA KUTENGENEZA MABATI NA BOMBA CHA ALAF PAMOJA NA KIWANDA CHA KUTENGENEZA MAFUTA YA KUPIKIA CHA MURZAH WILMAR. Kamati ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Viwanda, Biashara na Mazingira ikiongozwa na mwenyekiti wake ndugu Suleiman Ahmed Sadiq watembelea Kiwanda cha kutengeneza mabati cha Alaf pamoja na Kiwanda cha kutengeza mafuta ya kupikia cha Murzah Wilmar vilivyopo barabara ya Nyerere jijini Dar es salaam. Lengo la Ziara hiyo ilikuwa ni kusikiliza cha changamoto za wenye Viwanda mbalimbali ili Wizara husika kuzichukua na kuzifanyia kazi pia kamati ya bunge kuishauri serikali namna ya kuboresha changamoto husika ili kuvisaidia Viwanda vya ndani kuongeza uzalishaji, kuongeza ajira na kukuza uchumi.