Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Malawi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan afungua Kongamano la Biashara na Uwekezaji Baina ya Tanzania na Malawi na kuhimiza ushirikiano wa Kibiashara na Uwekezaji baina ya nchi hizi mbili. Kongamano limefanyika leo tarehe 26 Julai, 2018 katika ukumbi wa Tughimbe, Mkoani Mbeya.
Makamu wa Rais amesisitiza ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Malawi uendelezwe kwa makongamano mbalimbali kufanyika kwa kujadiliana jinsi ya kutatua changamoto zilizopo ili kurahisha biashara na uwekezaji baina ya nchi hizi mbili.