Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Habari

Serikali inahakikisha sekta binafsi inaendelea kukua na hakuna kiwanda chochote kitakachofungwa ili kuendelea kuongeza ajira na kukuza uchumi wa Taifa 


Waziri wa Viwanda Na Bishara Mhe Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) amesema 
Serikali inahakikisha sekta binafsi inaendelea kukua na hakuna kiwanda chochote kitakachofungwa ili kuendelea kuongeza ajira na kukuza uchumi wa Taifa 

Waziri Kijaji ameyasema hayo   Agosti 1, 2023 alipotembelea Kiwanda cha A to Z kilichopo jijini Arusha kwa lengo la kujionea shughuli za uzalishaji kiwandani hapo na kusikiliza na kitatua changamoto walizonazo.

Aidha,  Amewataka  wafanyabiashara kuwa na ushirikiano na Serikali katika kutoa changamoto wanazozipata na watoe  mapendekezo ya suluhisho za changamoto hizo  kwa kuwa Serikali ipo tayari kuzishughulikia