Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Habari

Serikali  ya Awamu ya Sita imedhamiria kuwanyanyua wanawake wajasiriamali nchini


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Hashil Abdallah amesema  Serikali  ya Awamu ya Sita imedhamiria kuwanyanyua wanawake wajasiriamali nchini kwa kuhakikisha wanapata elimu ya ujasiliamali  na kuendeleza  mawazo yao ya kibiashara.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji  wakati wa kufunga mafunzo ya wajasiriamali yaliyofanyika Juni 6, 2022 jijini Dodoma amesema ni wajibu wa wanawake kuchangamkia fursa hizo.

Kwa upande wake Mratibu wa  Programu ya kuwajengea uwezo wajasiriamali wanawake (Academy of Women Entrepreneurs – AWE) Tanzania Dkt. Victoria Kisyombe  pamoja na wanufaika 31 wa mafunzo hayo  maalum ya wiki 10 wameeleza  namna mafunzo hayo yanavyosaidia kukuza ujasiriamali nchini. 

Naye, Balozi wa Marekani nchini Mhe. Dkt. Donald Wright amesema Serikali ya Marekani imeongeza dola laki moja za ziada kufadhili mafunzo kwa wanawake wajasiliamali kwa mikoa minne mwaka 2023  nchini Tanzania na kueleza matokeo ya mafunzo hayo. 

 “Mafunzo ya wiki 10 mliyoyapata mkiwa sehemu ya programu hii yamewapa ujuzi kwa vitendo utakaowawezesha kuanzisha biashara endelevu pamoja na kuwaunganisha na wakufunzi (mentors) na wajasiriamali kama ninyi wa nchini Marekani,” alisema.

Washindi wanne bora katika mafunzo hayo ya ujasiriamali yaliyotolewa jijini Dodoma kwa wiki kumi na tatu watapatiwa mtaji wa dola elfu kumi ili kuendeleza mawazo yao ya kibiashara.