Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Habari

Wafanyabiashara wahimizwa kuchangamkia fursa AfCFTA


Mkurugenzi wa Idara ya Viwanda, Wizara ya Uwekezaji Viwanda na Biashara Dkt. Lugano awahimiza wafanyabiashara kuchangamkia fursa adhimu eneo la soko huru  la Biashara Afica - African Con betinental Free Trade Area (AfCFTA)  ili kuongeza uzalishaji na uongezaji wa thamani kwenye mazao,mifugo na uvuvi.
 
Dkt Lugano ameyasema hayo leo tarehe  13  April,2023  katika ukumbi wa hoteli ya Dodoma wakati akitoa mada kwenye  ufunguzi  wa kongamano la wadau wa sekta ya kilimo kwa niaba ya Katibu  Mkuu  Wizara ya Uwekezaji Viwanda na Biashara Dkt. Hashil Abdallah.

Kongamano hilo la tisa kufnyika linahusisha wadau wa sekta ya kilimo ili  kufanya  tathimini ya  matokeo ya tafiti na maboresho ya sera,kanuni na sheria katika sekta ya  kilimo ili kuweka mazingira  wezeshi yatakayoleta mageuzi katika sekta ya kilimo na mnyororo wa thamani pindi utekelezaji wake utakapoanza.

Aidha akizungumza katika kongamano hilo Dkt. Lugano amewaomba wafanyabiashara waliotayari  kufanya  biashara katika eneo la soko huru  la Biashara Africa -African Continental free Trade Area (AfCFTA) kubisha  hodi kati Wizara ya Uwekezaji Viwanda na Biashara kwa lengo kukuza uchumi wa nchi na uchumi wa wafanyabishara wetu. 

“Katika kujipanga serikali kwa sasa inaendelea kukamilisha mkakati wa kitaifa wa  utekelezaji  wa mkataba wa AfCFTA, wataalam wa wizara wapo Dar es Salaam wakishirikiana na sekta binafsi kwa lengo la kuweka mikakati bora na endelevu ya kuwezesha nchi yetu amesema” Dkt Lugano.

Kwa hiyo tunategemea kwamba mapendekezo yatakayotolewa katika mkutano huo  yatakuwa na tija , kubwa hivyo tuwaombe wadau wa biashara waliotayari kufanya biashara chini ya AfCFTA wasisite kutuona  ili tuweze kuwaunganisha katika  programu zinazoendea

Aidha Dkt. Lugano ameongeza kuwa  Tanzania  ni miongoni  mwa nchi saba ambazo zimeridhia mkataba huo na  kuwa miongoni mwa nchi  za awali ambazo zitanufaika  kupitia program iliyoanzishwa na sekretarieti ya AFCFTA .