Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Viwanda na Biashara

Habari

Waziri Kijaji : Ametembelea Bandari ya Tanga na kujionea shughuli za upanuzi wa bandari


Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) akiwa ameambatana na  Mkuu wa Mkoa Mhe. Adam Malima Mei 30, 2022  ametembelea Bandari ya Tanga na kujionea shughuli za upanuzi wa bandari hiyo  unavyoendelea ili kuiwezesha kupokea meli za mizigo  kubwa na kuwa na uwezo wa kuhifadhi mizigo mingi kwa wakati mmoja. Hii ni hatua ya Serikali katika kuweka mazinhira bora na wezeshi kwa wafanyabiashara na wawekezaji.